Sunday, 22 November 2015

BODI YA MIKOPO KWA ELIMU YA JUU (HESLB) YATOA TAARIFA MPYA KWA AMBAO HAWAJAAMBATANISHA BAADHI YA TAARIFA MUHIMU KWA BODI:


Taarifa inasomeka kuwa Bodi (HESLB) iko katika hatua za mwisho kuwapangia mikopo wanafunzi wote wa Elimu ya Juu walioomba kwa mwaka wa masomo wa 2015/2016. Na katika mchakato huo, Bodi imegundua kuwa wanafunzi waliotuma maombi wapatao 336 wanamapungufu katika Fomu zao za maombi ya Mkopo kwa kukosa nakala za Vyeti vya Kuzaliwa ili kubainisha na kuhalalisha Uraia/Utaifa wao.

Hivyo Bodi ya Mikopo (HESLB) inawahasa wote waliotuma maombi kwa mwaka wa masomo wa 2015/2016 kufika katika Ofisi za Bodi ya Mikopo kwa Elimu ya Juu (HESLB) Kitalu Namba 8, Nyumba Namba 46 Barabara ya Sam Nujoma, Mwenge - Dar es Salaam kwa ajili ya kuziwasilisha taarifa zao muhimu ikiwa ni pamoja na Nakala za Vyeti vyao vya Kuzaliwa . Ikumbukwe kuwa Bodi ilitoa siku kumi na nne (14) kwa wale wote ambao taarifa zao zilikua na makosa kuanzia Tarehe 27/08/2015 hadi Tarehe 11/09/2015 ili waweze kurekebisha makosa yote yaliyopatikana katika fomu zao za Maombi ya Mkopo.

Majina yote ya ambao taarifa zao hazijakamilika yanapatikana hapa.
Tarehe ya mwisho ya kukusanya hizo nakala za vyeti vya kuzaliwa ni Tarehe 30/11/2015 saa 11:00 Jioni. 

Imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu
Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB).

Na kutafsiriwa na Elirinyo Uronu.

 Taarifa ya awali katika tovuti ya Bodi
 
NOTICE TO LOAN APPLICANTS TO SUBMIT COPIES OF CERTIFIED BIRTH CERTIFICATES:
:
The Higher Education Students’ Loans Board (HESLB) is finalizing allocation of students’ loans for the 2015/2016 Academic Year. In the process, we have identified 336 eligible applicants whose loan application forms miss birth certificates to authenticate their nationality.
 Therefore, HESLB hereby calls upon loan applicants for academic year 2015/2016 whose names are appended herewith to physically come to HESLB offices on Plot No. 8, Block No. 46 Sam Nujoma Road, Mwenge - Dar es Salaam to submit their certified copies of birth certificates.  It should be remembered that, the Board had earlier on given loan applicants fourteen days starting from 27th August, 2015 to 11th September, 2015 to rectify anomalies found in their application forms.
 Names of concerned applicants can be accessed here
The deadline for submission of certified birth certificates is 30th November, 2015 at 5.00pm.

 

Issued by:
  Executive Director
  HIGHER EDUCATION STUDENTS’ LOANS BOARD



@RINYO'S

No comments:

Post a Comment