Katika kipindi hiki cha kuelekea mwishoni mwa mwaka basi la kampuni ya SIMBA MTOTO limepata ajali katika eneo la kwa Fundi katika mji mdogo wa TENGERU Jijini Arusha asubuhi ya leo, kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wanasema kuwa chanzo ni mwendo wa dereva wa basi hilo la mkoani ambalo lilikua likitokea Arusha kuelekea Dar es Salaam, ambapo wanadai kuwa dereva huyo alikua anaovertake na wakati huo huo gari aina yaa fuso lililokuwa likielekea Arusha mjini likiovertake pia ndipo dereva wa Simba Mtoto alipofanya juhudi za kukwepa kugongana uso kwa uso na Fuso hiyo jambo ambalo lilisababisha basi hilo kupinduka.
![]() |
| Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo wakilitazama basi hilo lililopinduka (Picha na Elirinyo). |
Hadi tunafika eneo la tukio mida ya saa 02:30 hatukuweza kukuta majeruhi wowote katika eneo la ajali, na mashuhuda wanasema kuwa majeruhi walikimbizwa Hospitali kwa ajili ya kupatiwa huduma ya kwanza na matibabu.
![]() |
| Basi la Simba Mtoto likiwa limepinduka katika eneo la TENGERU (Picha na Elirinyo) |
Bado tunaendelea kutafuta mawasiliano kutoka kwa Kamanda mkuu wa usalama katika mkoa wa Arusha Liberatus Sabasi ili kuweza kujua hali za majeruhi na kuweza kujua kama kuna yeyote aliyepoteza maisha.
![]() |
| Basi la Simba Mtoto kama linavyoonekana kwa mbele baada ya kupinduka (Picha na Elirinyo) |
![]() |
| (Picha na Elirinyo) |
@RINYO'S








