Na Elirinyo Uronu
Serikali ya wanafunzi ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAASO) kupitia kwa Waziri Mkuu wake Bw. Boniface Elibariki yatangaza rasmi kupunguza bei za Stationary Chuoni hapo. Akitoa tangazo hilo waziri mkuu wa Serikali hiyo ameeleza kuwa wamefanya hivyo ikiwa ni katika kutimiza moja kati ya ilani na ahadi walizokuwa wanazitoa wakati wa kampeni za kuomba ridhaa ya kuongoza chuoni hapo.
Bw. Boniface Elibariki ametanabaisha kwamba hatua hiyo itawawezesha wanafunzi kuweza kumudu gharama za maisha chuoni hapo ikiwa ni pamoja na gharama hizo za Stationary.
katika taarifa hiyo inaonyesha kuwa Bei za Kuchapa (Printing) zimeshuka kwa asilimia takribani 50% kutoka Tsh. 200/= hadi Tsh. 100/= kwa ukurasa huku gharama za kutoa nakala (Photocopying) zikishuka pia kwa assilimia 50% kutoka Tsh. 50/= kwa kurasa hadi Tsh. 25/=
![]() |
| Tangazo la bei mpya za Uchapaji na kutoa Nakala kama linavyoonekana |
@RINYO's
