Wednesday, 9 December 2015

CHUO CHA UHASIBU ARUSHA LEO HII KIMEKUMBWA NA SIMANZI KUBWA BAADA KUKUMBWA NA TANZIA YA VIJANA WAO WAWILI WA NGAZI YA SHAHADA (DEGREE).


Ulikua ni mchana mzuri wenye pilikapilika za hapa na pale huku ukihusisha pia maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Tanganyika ambayo yaliambatana na tukio la kufanya usafi katika maeneo ya majumbani na kazini pia kama utekelezaji wa Agizo la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.

Lakini siku haikuweza kuisha vizuri katika Chuo cha Uhasibu Arusha kwani mnamo majira ya saa 11 jioni zilianza kusambaa taarifa za uvumi wa vifo vya wanafunzi wawili, huku wanafunzi wengi wakiwa katika kuhamaki na wakipambana huku na kule ili kuupata ukweli juu ya taarifa hizi ndipo taarifa rasmi zilipotufikia kuwa wanafunzi wawili wa ngazi ya Shahada wa chuo Cha Uhasibu Arusha wamepata ajali katika barabara ya Njiro - Arusha karibu na Kituo cha Mafuta cha BP. Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wanasema kuwa ajali hiyo ilihusisha Pikipiki iliyokuwa ikitumiwa na wanafunzi hao pamoja na gari aina ya Land Cruizer, mashuhuda wanadai kuwa pikipiki hiyo iliyokuwa ikiendeshwa na Marehemu Carthbet Massawe iligongana na gari hilo na kusababisha ajali hiyo kutokea ambayo ilisababisha Carthbet kupoteza maisha hapohapo huku mwenzake ambaye ni Emmanuel Robson Sabuni akiwahishwa Hospitali kutokana na majeraha aliyoyapata lakini hata hivyo kwa taarifa tulizozipata kutoka Hospitali ni kuwa pia Emmanuel naye alifariki akiwa katika chumba cha wagonjwa Mahututi (ICU).

Kwa kweli vifo hivi vimepokelewa kwa simanzi kubwa hapa chuoni huku wengi wakiwa bado hawaamini kwa taarifa wanazozipata kutoka kwa Magroup yao ya Whatssap ya madarasani. Vijana hawa wametutoka wakiwa bado wadogo sana huku wakikadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 23 na 25, Marehemu Emmanuel Sabuni alikua ni mwanafunzi wa Shahada ya TEHAMA (BIT) mwaka wa kwanza huku mwenzake ambaye ni Marehemu Carthbet Massawe akiwa ni mwanafunzi wa Shahada mwaka wa pili.

Wote walikua ni watumishi wa Mungu katika Fellowship ya ICF hapa chuoni na walikua katika maandalizi ya sherehe ya Kidini ya kuwakaribisha wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza (ICF FRESHERS) ambayo ilitarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi Tarehe 12/12/2015.


Marehemu Emmanuel Sabuni katika enzi za uhai wake akiwa Madhabahuni.
Marehemu Emmanuel Sabuni akionekana katika moja ya Events alizoshiriki kuziandaa.
Marehemu Carthbet Massawe katika enzi za Uhai wake.
 Marehemu wote kwa pamoja wataacha pengo kubwa katika Fellowship ya ICF kwani walikua watu muhimu sana katika Team ya Maombi na Kwaya ya ICF, pia Marehemu Emmanuel ataacha pengo kubwa katika kanisa la KKKT alilokua anasali ambapo yeye alikua ni kiongozi wa kwaya.

Marehemu Carthbet Massawe na Marehemu Emmanuel Sabuni katika picha ya pamoja, Bwana ametoa na Bwana Ametwaa jina lake lihimidiwe. R.I.P Brothers.


Share na wengine ili tuzidi kuwaombea wapendwa wetu hawa walazwe mahali pema peponi.

@RINYO'S

UKAWA WAJAZANA MAHAKAMA ZA KANDA YA ZIWA KUTETEA NAFASI ZAO ZA UBUNGE:



KESI za kupinga matokeo ya ubunge zimezidi kumiminika katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mwanza, ikiwamo za kupinga matokeo yaliyompa ushindi Mbunge wa Bunda Mjini Ester Bulaya (Chadema)
Kesi nyingine zilizofunguliwa mahakamani ni za majimbo ya Nyamagana, Ilemela na jimbo la Kwimba, ambapo walalamikaji wamewasilisha malalamiko mbali mbali ikiwamo ya vitendo vya rushwa.

Kesi ya kwanza iliyofunguliwa ni ya ubunge wa Jimbo la Bunda Mjini ambayo imefunguliwa na Magambo Masato na wenzake watatu wakipinga matokeo yaliyompa ushindi Mbunge wa Jimbo hilo, Ester Bulaya.

Kesi hiyo namba 1 ya mwaka 2015 mara ya kwanza ilifunguliwa Novemba 18 mwaka huu, juzi ilikuwa mara ya kwanza kupelekwa mahakamani kwa ajili ya kutajwa.

Kesi hiyo ambayo ipo kwa Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mwanza, Francis Kabwe, walalamikaji wa kesi hiyo wamewasilisha malalamiko mahakamani hapo wakidai kwamba Bulaya alipata ushindi kwa njia ya rushwa.

Bulaya aweka pingamizi
Mlalamikiwa katika kesi hiyo, ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Ester Bulaya, mapema juzi aliwasilisha hoja za msingi kuweka pingamizi kwa walalamikaji kufungua kesi mahakamani.

Hoja alizowasilisha Bulaya ni kwamba walalamikaji hawana mamlaka ya kufungua na kuendesha kesi ya aina hiyo kwani hawajaonesha ni namna gani imeathiri haki zao kama wapiga kura.

Pili katika shauli walillowasilisha mahakamani hawakuonesha ni namna gani vitendo vya rushwa walivyodai vilikuwa vikifanywa na Mawakala wa Bulaya havijaoneshwa, pia shauri hilo limekiuka kifungu cha 12 (D) cha sheria ya uchaguzi.

Hata hivyo kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba 29 mwaka huu, itakapo tajwa tena mahakamani hapo kwa ajili ya kuisikiliza.

Kesi ya Wenje
Aliyekuwa Mgombea ubunge Jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza, Ezekiah Wenje, juzi alitinga Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mwanza, kuomba kupunguziwa gharama za uendeshwaji wa kesi.

Pia Wenje katika kesi hiyo anawashitaki, Mbunge wa Nyamagana Stanslaus Mabula (CCM), Msimamizi wa Uchaguzi huo, Tito Mahinya na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Hata hivyo amewasilisha malalamiko mahakamani hapo kwamba uchaguzi huo haukuwa haki na huru, kwenye uchaguzi uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu.

Hata hivyo katika kesi hiyo namba 3 ya mwaka 2015, Wenje aliwakilishwa mahakamani hapo na Wakili Outa na upande wa walalamikiwa waliwakilishwa na Wanasheria wa Serikali, Mtalemwa, Kitia Tuloke na Ajuaye Bilishaga.

Kesi ya Highness Kiwia
Novemba 25 mwaka huu aliyekuwa mgombea ubunge Jimbo la Ilemela, Highness Kiwia, alifungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mwanza ya kupinga matokeo yaliyompa ushindi, Angelina Mabula (CCM) pamoja na kuwashitaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Msimamizi wa Uchaguzi huo, John Wanga.

Kesi hiyo namba 2 ya mwaka 2015, mlalamikaji katika kesi Kiwia hakufika mahakamani hapo, ambapo kwa upande wa walalamikiwa waliwakilishwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Malongo.

Kesi ya Wenje na Kiwia zimeahirishwa ampapo ya Wenje itatajwa Desemba 10 mwaka huu na ya Kiwia hadi Desemba 14 mwaka huu, huku Msajili, Kabwe amedai kuwa endapo siku hiyo mlalamikaji Kiwia hatatokea kesi itatupiliwa mbali.
 
 
@RINYO'S
LEO NI SIKU MUHIMU SANA KWA NCHI YETU KWA KUTIMIZA MIAKA 54 TANGU ILIPOJIPATIA UHURU WAKE MNAMO TAREHE 09/12/1961.


Lakini leo hii Rais wa Awamu ya Tano Mh. Dkt. John Pombe Magufuli ameamua watu wote waadhimishe siku hii kwa kufanya usafi katika makazi yao na maeneo yao ya kazi ili kuweza kukabiliana na Ugonjwa wa KIPINDUPINDU, zoezi hilo limeanza kutekelezwa asubuhi hii ya leo huku Mh. Rais akiliongoza kwa kufanya usafi katika eneo la Soko la Feri .

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Janeth akiongoza zoezi la kufanya usafi katika Soko la Feri.


Rais mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiongoza wananchi wa eneo chalinze kufanya usafi
Kama hiyo haitoshi pia wasanii na baadhi ya vituo vya Redio vikiongozwa na Clouds Media Group wameshiriki katika kufanya usafi ikiwa ni njia ya kutekeleza agizo la mheshimiwa Rais.



Watangazaji wa kipindi cha Leo Tena cha Clouds Fm #TeamLeoTena wakiwa katika mavazi ya usafi kwa ajili ya kulitimiza agizo la Rais. (Dahuu, Musa Husein, Jose Mara, Ge Habibu nk.)

Katika kufanya usafi huku kumeibua mengi hapa ni watangazaji wa Clouds Fm wakitoa meno ya Ng'ombe ambayo yalikua yamehifadhiwa kwa takribani miezi sita kwa bibi mmoja mkazi wa Tandale ambayo yalikua yakiwasababishia majirani kero.

Staa wa bongo Fleva Tundaman akiwa na Team Leo Tena ya Clouds wakifanya usafi eneo la Soko la Tandale.

Pia Taasisi mbalimbali zimeonyesha kuunga mkono kauli ya Rais ya kufanya usafi ikiwa ni pamoja na Hospitali ya Rufaa ya SEKOTOURE iliyoko jijini Mwanza pia Taasisi za Elimu ya juu ikiwa ni pamoja na Chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM nacho kimeunga agizo la Mh. Rais kwa asilimia 100 na katika mbao zake za matangazo kulisomeka hivi.

Tangazo katika mbao za matangazo za Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) kama linavyoonekana.


Mwanafunzi wa Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM) aliyefahamika kwa jina moja la Shangwe akivaa Gloves tayari kwa kazi ya utekelezaji wa agizo la Rais la kufanya usafi.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya SEKOTOURE Jijini Mwanza wakiwa na vifaa vya kufanyia usafi tayari kutekeleza agizo la Rais.






Usisahau kutoa maoni yako juu ya maamuzi haya ya Rais na pia kuhusiana na mwitiko wa wananch katika eneo lako

@RINYO'S