Sunday, 20 March 2016

SIASA:

CCM HIVI LEO YATANGAZA MSEMAJI WAKE MPYA:

Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na kushoto ni aliyekuwa Katibu Mwenezi wa chama hicho Ndugu Nape Nnauye ambapo kwa sasa Olesendeka pichani kati ndiye ameishika nafasi hiyo.

Chama cha Mapinduzi CCM leo kimemtangaza Christopher Ole Sendeka kuwa msemaji mpya wa CCM kuanzia leo.Sendeka ametangazwa rasmi na Katibu Mkuu wa chama hicho Ndugu Abdulrahman Kinana mbele ya Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam.


Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimtangaza Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Christopher Ole Sendeka kuwa Msemaji Rasmi wa CCM leo, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam 


Msemaji mpya wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Christopher Ole Sendeka akiongea baada ya kuteuliwa siku ya leo. kulia ni aliyekua katibu mkuu mwenezi Ndugu Nape Nauye.

 @RINYO'S