Wednesday, 2 December 2015

SERIKALI YA KOREA YAFUNGUA RASMI NA KUKABIDHI JENGO LA MICHEZO YA TAEKWONDO KWA JESHI LA POLISI LA TANZANIA:

Serikali ya Korea ikiwakilishwa na Balozi wake Mh. II Chung katika kuboresha mahusiano mema na Serikali ya Tanzania hiyo jana ilifanikiwa kuzindua Jengo maalumu kwa ajili ya Michezo ya Taekwondo na kulikabidhi Jeshi la Polisi lililowakilishwa na Naibu Mkuu wa Jeshi Nchini DIGP Abdulrahman Kaniki akiongozana na maafisa mbalimbali wa Jeshi la polisi.


Naibu Mkuu wa Jeshi Nchini DIGP Abdulrahman Kaniki na
Balozi wa Korea hapa nchini Mh. II Chung wakikata utepe kuashiria kufunguliwa rasmi kwa jengo la kisasa la michezo ya Taekwondo ambalo lilimekabidhiwa kwa jeshi la polisi nchini.
 

Naibu Mkuu wa Jeshi Nchini DIGP Abdulrahman Kaniki na
Balozi wa Korea hapa nchini Mh. II Chung katika picha ya pamoja na timu ya Taekwondo baada ya makabidhiano ya Jengo hilo la kisasa tukio lililofanywa na Balozi wa Korea nchini.



Naibu Mkuu wa Jeshi Nchini DIGP Abdulrahman Kaniki akimkabidhi cheti Bw, Shieyoung Pyeon baada ya makabidhiano ya jengo la michezo ya Taekwondo.


@RINYO'S 

Usisahau kuweka maoni yako hapaaaa....... 

No comments:

Post a Comment