Tuesday, 1 December 2015


ALLY KIBA NDANI YA SOUTH AFRIKA TENA JE TUSUBIRI NINI KIPYA KUTOKA KWAKE??

AC8U4832-1

Staa wa muziki wa Bongo Fleva Ali kiba ametinga tene ndani ya South Africa kwa  mara nyingine, hii sio safari ya kwanza kwenye siku za hivi karibuni japo safari za kwanza na hii ya sasahivi ziko tofauti kidogo..
Ali kiba ana kazi nyingine iliyomfanya akatua South Africa kwa mara nyingine.
Ali kiba yuko South Africa toka November 29 2015 akiwa kama Balozi wa kupingana na ujangili… kilichompeleka South Africa ni ishu ya kushiriki kongamano linalowakutanisha watu mbalimbali ikiwemo Wakurugenzi mbalimbali kutoka China na Africa pamoja na viongozi wa taasisi za kijamii, na kati ya mambo yatakayojadiliwa ni pamoja na njia bora za kusaidia utunzaji wa wanyamapori pamoja na hifadhi.
Katika maneno ambayo Ali Kiba aliyaongea alipotoa ujumbe wake akiwa South Afrika ni pamoja na na nanukuu
Nchi yangu imepoteza tembo wengi sana ndani ya miaka michache iliyopita kwa sababu ya ujangili… ni lazima tuangalie njia za kushirikiana kuhakikisha tunazuia mauaji hayo na kulinda wanyamapori wetu.”

Pia Kiba ambaye ni staa wa ngoma ya Nagharamia alisema
 
Sote tuna majukumu kuhakikisha tunalinda wanyamapori wetu, mimi kama msanii na mwanamuziki natumia nafasi yangu kusimamia suala hili na kuhimiza watu wengine wengi zaidi waunge mkono hizi jitihada.”
Alikiba ni Balozi wa WildAid Campaign ambayo inapiga vita ujangili ambapo mwanzo wa November 2015 alikuwa Marekani ambako alikutana na Mabalozi wengine kama akina Fergie, Lupita Nyong’o, na mastaa wengine wakubwa Duniani… ziara hii ya Alikiba itaendelea mpaka December 03 2015 na kati ya maeneo ambayo atatembelea ni pamoja na hifadhi ya wanyama ya Kruger National Park.


@RINYO'S.

No comments:

Post a Comment