Thursday, 11 February 2016

BURUDANI:



HARMONIZE AJICHORA TATOO YA PICHA YA DIAMOND:



Picha: Harmonize achora tattoo ya picha ya boss wake Diamond na kuandika ‘Simba’ 


Msanii wa label ya WCB anayekuja juu kwa sasa, Harmonize ameamua kuuthibitishia ulimwengu kuwa anajivunia kuwa mtoto wa kimuziki wa staa wa Tanzania, Diamond Platnumz kwa kuchora tattoo yenye picha yake na kuandika a.k.a ya Boss wake iliyozua utata hivi karibuni ‘Simba’. Hiki ndicho alichokiandika Harmonize kwenye picha aliyoipost Instagram kuelezea sababu za kuchora tattoo hiyo: 

“Katika Maisha Yangu Sikuwahi Kuwaza Kuwa Itatokea Siku Nikajichora Tatoo But Diamond Nimtu Mwenye Mchango Mkubwa Sanaaaa Katika Maisha Yangu Leo Hii Mimi Ninathaminika Kutoka Kwenye Kunyanyasika Ninaheshimika Kutoka Kwenye Kudhalaulika Nimekuwa Maarufu Na Kupata Uthamani Mkubwa Kupitia Yeye Siotu Kwa Kipaji Nilicho Nacho Kwani Wangapi Wanavipaji…??? Naisaidia Familia Yangu Kwa Kile Nikipatacho Sihaba Akiwa Na Mchango Wake Mkubwa Sana…… Lakini Mwisho Wasiku Haya yote ni kwaajili ya kuonyesha kuwa nauthamini sana msaada wake wa hali na mali"

Alisema hayoHarmonize.


@RINYO'S

No comments:

Post a Comment