Friday, 1 January 2016

SALAMU ZA MAGUFULI KWA MWAKA 2016

RAIS WA TANZANIA Dr. JOHN POMBE MAGUFULI AWAAPISHA MAKATIBU WAKUU WA WIZARA MBALIMBALI LEO IKULU DAR ES SALAAM...................


Wakati watu wengi duniani kote wakiwa bize na sikukuu ya Mwaka mpya ambayo imekua ni sikukuu ambayo imekua ikiadhimishwa na familia nyingi ulimwenguni kwa kukaa na ndugu zao pamoja na jamaa na marafiki na kujumuika katika kusherehekea, leo Rais mpya wa Tanzania wa Awamu ya Tano ameenda tofauti kwa kuingia ofisini (Ikulu) na kuwaapisha Makatibu wakuu na manaibu wao wa Wizara mbalimbali na kuudhihirishia umma kuwa kweli "Hapa ni Kazi Tu".

Katika hafla hiyo Rais Dr. Magufuli amewaapisha Makatibu wakuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Katibu mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Naibu katibu mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango,Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje,Afrika Mashariki,Kikanda na Kimataifa,Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,Profesa James Epifani Mdoe akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.John Pombe Joseph Magufuli na Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue wakati wa hafla ya kuwaapisha Makatibu Wakuu na Manaibu wao iliyofanyika katika Ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Jaji Meja Jenerali Projest A.Rwegasira akila kiapo cha utii  wakati wa hafla ya kuwaapisha Makatibu Wakuu na Manaibu wao iliyofanyika katika Ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam.

aibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria,Amon Mpanju akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.John Pombe Joseph Magufuli na Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue wakati wa hafla ya kuwaapisha Makatibu Wakuu na Manaibu wake iliyofanyika katika Ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango,Amina H.Shaban akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.John Pombe Joseph Magufuli na Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue wakati wa hafla ya kuwaapisha Makatibu Wakuu na Manaibu wao iliyofanyika katika Ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam.


Ukumbi wa Ikulu ya Dar es Salaam kama unavyoonekana wakati wa hafla ya kuwaapisha Makatibu wakuu wa Wizara mbalimbali na Manaibu.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi,Profesa Simon S.Msanjila akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.John Pombe Joseph Magufuli na Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue wakati wa hafla ya kuwaapisha Makatibu Wakuu na Manaibu wake iliyofanyika katika Ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam.

Pichani kuliani ni Makamau wa Rais Mh.Samia Suluhu Hassan akiteta jambo na Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Makatibu Wakuu na Manaibu wao Ikulu jijini Dar,wa tatu kulia ni Mke wa Rais,Mama Janeth Magufuli pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Bwa.George Masaju.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa,Immaculate Peter Ngwale akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.John Pombe Joseph Magufuli na Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue wakati wa hafla ya kuwaapisha Makatibu Wakuu na Manaibu wake iliyofanyika katika Ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam.

@RINYO'S

1 comment: