UDAKU:
NUHU MZIWANDA Akiri kuficha mambo mengi Mabaya ya Shilole ili kulilinda penzi lao......
NUHU MZIWANDA Akiri kuficha mambo mengi Mabaya ya Shilole ili kulilinda penzi lao......
Mastaa wa ngoma ya "Ganda la ndizi" waliokuwa wapenzi hapo awali Nuhu Mziwanda na Shilole wazidi kuibua makubwa katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya 'Bongo Fleva' ambapo Ijumaa ya wiki hii Nuhu Mziwanda alitoa mazito ya moyoni katika mahojiano ya live katika kituo cha Luninga cha Clouds TV.
Nuhu Mziwanda aliyasema hayo live siku ya Ijumaa ya Tarehe 15/01/2016 katika kipindi cha D'Weekend kinachorushwa live na Clouds Tv siku za Ijumaa, na maneno hayo aliyasema mbele ya Ex-Girlfriend wake Shilole "Shishi Baby" ambaye alikua amejikunyata pembeni kutokana na kukasirishwa na kitendo cha uwepo wa Ex-Boyfriend wake bila na kuwa na taarifa za awali.
Katika mahojiano hayo Nuhu alisema Shilole hakuwa mwanamke wa kutawaliwa, siku zote alijiona yeye ndo mwenye mamlaka ya kufanya maamuzi.
"Yeye anajua mambo gani ambayo alikua ananifanyia ambayo hakustahili kabisa yeye kunifanyia. Alikua anafanya kwa kunichukulia poa kwamba nitafanya nini lakini at the end of the day kila kitu kina mwanzo na mwisho" Alisema
![]() |
| Nuhu Mziwanda na Shilole wakiwa katika pozi matata wakati wa mahusiano yao. |
Nuhu alisema pia ni vigumu kwake yeye kurejesha imani kwa mpenzi wake wa zamani huyo japo pia amekiri kutokuwa tayari kuingia katika mahusiano na mwanamke mwingine yeyote.
Hivi karibuni pia Shilole aliwahi kuhojiwa na vyombo kadha wa kadha vya habari na kukiri kuwa yaliyotokea kati yake na Nuhu ni mazito.
![]() |
| Nuhu Mziwanda na Shilole wakati wakiwa wapenzi. |
@RINYO'S



No comments:
Post a Comment