Sunday, 24 January 2016

MATUKIO YA WIKI KITAIFA:

1. RAIS MAGUFULI AZIDI KUWA GUMZO NCHINI:




Mnamo Tarehe 20/01/2016 Mh. Dkt. John Pombe Magufuli anaonyesha ujuzi wake wa kutumia Cherehani
 

ANGALIA PICHA ZA RAIS DR. MAGUFULI AKISHONA NGUO KWA CHEREHANI...!!!


 Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli akionesha umahiri wake wa kutumia Cherehani na kushona nguo za wafanyakazi wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kuvifahamu vitengo mbalimbali na watumishi wake wa  Ikulu jijini Dar es salaam jana Januari 20, 2016.
 


2: WAZIRI MKUU AFUNGUA MKUTANO MKUU WA BUNGE LA AWAMU YA TANO DODOMA:

Tarehe 22/01/2016

Kwa mara nyingine tena shughuli za Bunge zinaanza upya baada ya kufunguliwa na Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa.


 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua mkutano wa wabunge, bungeni mjini Dodoma Januari 22, 2016.  Kulia ni Spika wa Bunge Job Ndugai na kushoto ni Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kahilillah
 Wabunge, Jenista Mhagama wa Peramiho (kushoto) na January Makamba  wakiteta katika mkutano wa wabunge, bungeni mjini Dodoma
  Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Gerge Masaju akitoa mada katika mkutano wa wabunge , bungeni mjini Dodoma Januari 22, 2016.


 Spika wa Bunge Job Ndugai akizungumza kumkaribisha Mwenyekiti wa Mkutano wa Wabunge, Waziri Mkuu, Kassim Majliwa kufungua mkutano huo bungeni mjini Dodoma Januari 22, 2016. Kulia ni Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashilillah.

  Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akisalimiana na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Januari 22, 2016.


3: RAIS MH. MAGUFULI ATINGA MAGWANDA YA JESHI LA WANANCHI TANZANIA (JWTZ) AKIWA JIJINI ARUSHA:

Tarehe 22/01/2016.

Tukio hili lilizua gumzo kubwa sana mitandaoni na hii ni baada ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli kuamua kuvaa mavazi ya kijeshi alipokua kwenye ziara yake Jijini Arusha. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wananchi wa Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha waliojitokeza kumsalimia wakati akielekea Monduli kwa ajili ya kufunga zoezi la Onesha uwezo Medani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa Mbauda Mkoani Arusha hawaonekani pichani wakati akielekea Monduli kwa ajili ya kufunga zoezi la Onesha uwezo Medani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisoma bango alilokabidhiwa na mwananchi mmoja katika eneo la Kona ya Nairobi Mkoani Arusha.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa Arusha katika eneo karibu na chuo cha Arusha Tech. Wananchi hao walifunga barabara ili wapate nafasi ya kumuona Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Mianzini Mkoani Arusha.
 Umati mkubwa uliojitokeza katika eneo la Mianzini Mkoani Arusha
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Nchini General Davis Mwamunyange wakati waufungaji wa zoezi la Onesha Uwezo Medani lililofanyika Monduli nje kidogo ya Jiji la Arusha.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Nchini General Davis Mwamunyange wakati akielekea kupewa maelezo ya zoezi zima la Onesha Uwezo Medan.


4: ALIYEKUWA KATIBU MKUU WA BARA LA AFRIKA DR. SALIM AHMED SALIM AZINDUA KITABU: 



Dkt. Salim Ahmed Salim (kulia), na Mwakilishi wa Kituo cha Kutatua Migogoro Barani Afrika, (Centre for Humanitarian Dialogue-CHD), Bw. Mohamed Omary wakionyesha Fremu yenye Mashairi ya kumsifu Dkt. Salim, huku Waziri Mahiga akishuhudia tukio hilo.
Hivi ndivyo uso wa kitabu hicho unavyoonekana.
Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb), ambaye ndiye alikuwa Mgeni Rasmi katika hafla ya uzinduzi wa kitabu cha Dkt. Salim Ahmed Salim (Salim Ahmed Salim: Son of Afica),akimzungumzia historia iliyotukuka ya Dkt. Salim Ahmed Salim, kabla ya uzinduzi wa kitabu hicho.

Dkt. Salim Ahmed Salim, akitoa maneno ya Shukrani kwa heshima aliyopewa kwa Mwandishi wa kitabu hicho lakini kwa wadau wote waliohudhuria hafla hiyo ya uzinduzi wa kitabu chake. Aliyekua Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (Katikati), akiwa na wageni mbalimbali wakati wa uzinduzi wa kitabu hicho. 
 
Waziri Mahiga akifurahia jambo na Dkt. Salim.

5: RAIS MH. MAGUFULI AWATUNUKU KAMISHENI MAAFISA WA JESHI HUKO MONDULI:

 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Majeshi Nchini Jenerali Davis Mwamunyange wakati alipowasili  katika chuo cha Maafisa wa Kijeshi Monduli Mkoani Arusha kwa ajili ya kuwatunuku Kamisheni Maafisa wapya wa Jeshi kwa cheo cha Luteni Usu, anayetazama katikati ni Mkuu wa Chuo hicho Meja Jenerali Paulo Peter Massao. 


 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipungia mkono wananchi wakati akiwasili kwenye viwanja vya Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli kwa ajili ya kuwatunuku Kamisheni Maafisa wapya wa jeshi kwa cheo cha Luteni Usu.




 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipigiwa wimbo wa Taifa kabla ya kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi katika viwanja vya Chuo hicho.



 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gwaride kabla ya kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya


 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia gwaride lililokuwa likipita mbele yake  kutoa heshima.


 Gwaride la Wahitimu likipita kutoa heshima mbele ya mgeni rasmi  Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli .
@RINYO'S

No comments:

Post a Comment